WIKI YA UTUMISHI WA UMMA-MAFINGA TC
“Lengo la Wiki hii ya maadhimisho ya Utumishi wa Umma ni kukumbushana wajibu na haki za watumishi wa Umma katika kuwaletea wananchi maendeleo hasa katika sekta ya kutoa huduma bora kwa wananchi”
Hayo yamesemwa na Mkuu wa Idaia ya Utawala na Rasilimali watu Halmashauri ya Wilaya ya Mji Mafinga Ndugu, Fredrick Kayombo alipokuwa akizungumza na watumishi wa kada mbalimbali katika Kata ya Isalavanu katika maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma ambapo kwa mwaka huu maadhimisho hayo yamefanyika kuanzia tarehe 16/6-23/6.
Amesema watumishi wanapodai haki zao pia wanatakiwa kukumbuka kutimiza wajibu wao, Hivyo wadai haki na kutimiza wajibu kwani lazima watumishi wapimwe kila mwaka kuona kuwa je wanatimiza wajibu wao?
Kata ya Bumilayinga pia ilitembelewa na Idara ya Utumishi, Elimu Msingi na Elimu Sekondari ambapo watumishi hao walipongeza uongozi wa Mji Mafinga kuadhimisha wiki ya Utumishi wa Umma kwa kuamua kuwafuata watumishi walio pembezoni kusikiliza kero zao na, kuwakumbusha wajibu wao kama watumishi wa Umma.
Bwana Kayombo amesema kuwa watahakikisha kata zote zinafikiwa na elimu inatolewa kwa watumishi wote kuwakumbusha kuhusu wajibu wao katika kuwahudumia wananchi.
Ametaja sababu ambazo zinaweza kupelekea Mtumishi wa Umma kufukuzwa kazi ni pamoja na Wizi, Utoro kazini, Ulevi mahala pa kazi, Uzembe, Kuaibisha utumishi wa umma na Ukaidi /dharau.
IMEANDALIWA NA OFISI YA HABARI NA MAWASILIANO
Sima Bingileki
Afisa Habari Mkuu
Mafinga Town.
Postal Address: Po.Box 76 Mafinga
Simu: +255 262 772 393
Mobile: 026-2772393
Barua Pepe: td@mafingatc.go.tz
Copyright ©2018 Mafinga Town Council . All rights reserved.