Kikao cha kwanza Cha Baraza la Halmashauri ya Mji Mafinga Kimefanyika na kuhudhuriwa na Mhe.Mbunge Dickson Lutevele,Jasmine N’gumbi Mbunge wa Vijana Viti Maalumu, Madiwani ,Wakuu wa Idara, Kamati ya Ulinzi na Usalama na Wageni waalikwa na kufanya Uchaguzi wa Mwenyekiti na Makamu Mwenyekiti, Uundaji wa Kamati za kudumu na kupitisha ratiba ya Vikao vya Halmashauri.
Mhe.Mbunge Lutevele amewashukuru Wananchi wa Mji wa Mafinga kwa kumchagua pia ameahidi kuonyesha Ushirikiano na amefungua milango ya Huduma wakati wote katika Ofisi yake.
“Katika Baraza tumepata Mwenyekiti Bora hivyo tujitahidi kufanya nae kazi kwa Ushirikiano lakini pia naomba niwape ahadi ya kuwa Mtumishi Mwema na nitashirikiana na nyinyi katika kuleta Maendeleo ya Jimbo letu la Mafinga”. amesema Mhe.Lutevele.
Akiongoza kikao Cha Baraza katika Ukumbi wa Halmashauri ya Mji Mafinga Katibu Tawala wa Wilaya ya Mufindi Ndugu Reuben Chongolo amewasihi Madiwani kufanya kazi kwa bidii, kusikiliza na kutatua Kero za Wananchi na kuwa kiungo kati ya Halmashauri na Wananchi ili kupata Amani na Taifa Bora.
“Mkatoe Huduma Bora kwa Wananchi kwa kusikiliza kero zao na kuzitatatua, kusimamia Miradi ya Maendeleo na Kukusanya Mapato ya Halmashauri katika Kata zenu na tunahitaji Mawazo yenu ili Kuboresha zaidi Ukusanyaji wa Mapato Bora utakaosaidia kupata Hadhi ya kuwa Manispaa”. amesema Ndugu Chongolo.
Naye Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Mafinga Bi; Fidelica Myovella amewapongeza Wabunge na Madiwani kwa kuchaguliwa na ameahidi kutoa Ushirikiano na Kutekeleza Ilani ya Chama Cha Mapinduzi kwa kufuata maelekezo kutoka Serikali kuu na kuyafanyia kazi ili kuleta Maendeleo ya Halmashauri ya Mji wa Mafinga.
Vedasto Faustine Malima
Afisa Habari
Mafinga Town.
Postal Address: Po.Box 76 Mafinga
Simu: +255 262 772 393
Mobile: 026-2772393
Barua Pepe: td@mafingatc.go.tz
Copyright ©2018 Mafinga Town Council . All rights reserved.