Umoja wa wafanyabiashara wa mazao yatokanayo na misitu katika Halmashauri ya Mji wa Mafinga Uwasa leo umekabidhi mitungi saba ya gesi,luninga moja pamoja kompyuta mpakato moja kwa Mkuu wa wilaya ya Mufindi Mh Saad Mtambule.
Akikabidhi vifaa hivyo Mwenyekiti wa wafanyabiashara hao ndugu Christian Ahia amesema vifaa hivyo vimepatikana kwa kushirikiana na wadau wao ambao ni shamba la miti Sao Hill kupitia wakala wa misitu Tanzania (TFS) ambapo mitungi saba itatumika katika hospitali ya Mji wa Mafinga na luninga pamoja na kompyuta mapakato vimeelekezwa kwa gereza la Isupilo kwa lengo la kuwezesha upatikanaji wa mfumo wa kitehama na kufuatilia rufaa na mashauri mbalimbali Mahakamani.
Vifaa hivyo vyenye thamani ya shilingi milioni sita na laki tatu vyote kwa pamoja vimepokelewa na kukabidhiwa kwa taasisi husika tayari kwa matumizi,akipokea vifaa hivyo Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji wa Mafinga bi. Happiness lazier aliwashukuru wadau hao na kuwapongeza kwa namna walivyounga mkono mapambano dhidi ya ugonjwa wa uviko-19 hali hadhalikka nae Mh. Mkuu wa wilaya ya Mufindi aliupongeza umoja huo wa wavunaji wa mazao ya misitu kwa kuunga kuungana na Serikali katika mapambano hayo dhidi ya ugonjwa wa uviko -19.
Mafinga Town.
Postal Address: Po.Box 76 Mafinga
Simu: +255 262 772 393
Mobile: 026-2772393
Barua Pepe: td@mafingatc.go.tz
Copyright ©2018 Mafinga Town Council . All rights reserved.