KILELE CHA WIKI YA UTUMISHI WA UMMA KIMEHITIMISHWA KWA WATUMISHI WA MJI MAFINGA KUFANYA USAFI WA MAZINGIRA KATIKA HOSPITALI YA MJI MAFINGA NA KUKUMBUSHANA HAKI NA WAJIBU WA MTUMISHI WA UMMA.
“Ni wajibu wetu sisi watumishi wa Umma kuwa Mabalozi wazuri katika utunzaji wa Mazingira, tukiona mtu anatupa taka hovyo hebu tumuambie kuwa sio sawa, taka ziwekwe sehemu sahihi na tuwe na utamaduni wa kuchukia taka, ukimaliza matumizi ya chochote ulichonacho kama mabaki hakikisha unakihifadhi sehemu iliyotengwa kuhifadhi taka”
Kauli hiyo Imetolewa na Bwana Charles Tuyi alipokuwa akimwakilisha Mkurugenzi wa Mji Mafinga Bi Happiness Laizer kwenye Kilele cha Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma ambayo ilianza tarehe 16/6 na kuhitimishwa tarehe 23/6/2022.
Amesema Kitu chochote kikiwakipo sehemu ambapo hakitakiwi kuwa ni uchafu, tujitahidi kutunza mazingira, kwenye maeneo ya mikusanyiko ya watu kama mahospitalini, sokoni, stendi na wale wanaohusika na utunzaji wa mazingira basi wajitahidi kando kando ya barabara kuwe kusafi.
Akiwakumbusha watumishi wa Umma kuhusu wajibu wao Mkuu wa Idara ya Utawala na Rasilimali watu Bwana Fredrick Kayombo amesema kuwa Watumishi lazima watimize wajibu wao kwani. Wajibu na haki ni vitu vinavyoenda pamoja.
Masuala yote ya Elimu, Kupandishwa vyeo, kulipwa stahiki zote kwenda Likizo ni haki ya mtumishi, lakini unapodai haki zako hakikisha na wewe unatimiza wajibu wako, kwa kuwahi kazini, kufanya kazi kwa kujituma na ubunifu, kutoa huduma bora na haki kwa mwananchi yeyote unayemhudumia.
Idara ya Utumishi katika wiki hili la Utumishi wa Umma iliweza kuwatembelea watumishi wa Mafinga Mji wanaofanya kazi ngazi ya Kata katika sekta zote.
Baadhi Kata zilizotembelewa ni Bumlayinga, Saohill, Isalavanu na Rungemba.
Imeandaliwa na Ofisi ya Habari na Mawasiliano
Sima Bingileki
Afisa Habari Mkuu.
Mafinga Town.
Postal Address: Po.Box 76 Mafinga
Simu: +255 262 772 393
Mobile: 026-2772393
Barua Pepe: td@mafingatc.go.tz
Copyright ©2018 Mafinga Town Council . All rights reserved.