“ Shule hii Shikizi ya Maarifa inaende kusajiliwa kuwa rasmi Shule ya Msingi na Mwaka 2026 itapokea wanafunzi kwani ni Shule inayojengwa kwa Mapato ya Ndani na kwa sasa matundu ya vyoo yanajengwa na mpaka kufikia mwezi wa 12 matundu ya vyoo 12 kwa wavulana na wasichana yatakuwa yamekamilika pamoja na choo cha walimu ambapo tumepeleka kiasi cha Shilingi milioni 44 kutoka mapato ya ndani”

“Shule nyingine Shikizi ambazo mwaka 2026 zitapokea rasmi wanafunzi ni Shule Shikizi ya Mshkamano na Itamba, ndio maana Halmashauri ikileta tu fedha ngazi ya Katq
Kwaajili ya utekekezaji wa Miradi lazima Timu ya Menejimenti ifanye ziara ya Ufuatiliaji ili kuhakikisha fedha Ilizoletwa ngazi ya Kata zinatekekeza Mradi husika “ Amesema Bi. Myovella
Nae Afisa Mipango wa Mji Mafinga Ndugu. Peter Ngusa amesema Halmashauri imekuwa ikipeleka fedha za Utekelezaji wa Miradi ya Maendeleo ngazi ya Kata na kwa kufuatilia mara kwa mara Utekekezaji wa Miradi kunafanya Miradi kukamilika kwa wakati na kwa ubora Mkubwa.

Aidha Mkurugenzi Mji Mafinga Bi. Fidelica Myovella akiwa ameongozana na Wakuu wa Idara wamefanya ufuatiliaji wa Miradi ya Maendeleo lengo likiwa ni kushauri na kusukuma ukamilishaji wa Miradi ya Maendeleo inayotekelezwa katika ngazi ya Kata.
Miradi iliyotembelewa ni Mradi wa Ujenzi wa Shule Mpya ya Sekondari ya Amali katika ukamilishaji wa Bwalo la Chakula ambapo ujenzi wake umegharimu kiasi vha shilingi Bilioni 1.6 kutoka Serikali Kuu, Shule Shikizi ya Maarifa na Shule mpya ya Sekondari ya Kata Mgodi iliyogharimu kiasi cha shilingi Milioni 583.18 fedha kutoka Serikali Kuu.

Sima Bingileki
Afisa Habari Mkuu- Mafinga Tc
Mafinga Town.
Postal Address: Po.Box 76 Mafinga
Simu: +255 262 772 393
Mobile: 026-2772393
Barua Pepe: td@mafingatc.go.tz
Copyright ©2018 Mafinga Town Council . All rights reserved.