• Malalamiko |
    • Wasiliana na sisi |
    • Maswali |
    • Baruapepe |
Mafinga Town Council
Mafinga Town Council

Jamhuri Ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Mafinga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Organization Structure
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Kilimo na umwagiliaji
      • Fedha
      • Mipango na Takwimu
      • Elimu ya Sekondari
      • Elimu ya Msingi
      • Afya
      • Ardhi na Maliasili
      • Community Development,Social welfare Gender and Youth
      • Water
      • Work
    • Vitengo
      • Community
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Huduma za Kisheria
      • Biashara
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa madiwani
    • Kamati Za Kudumu Za Halmashauri
      • Fedha Na uongozi
      • Mipangomiji Namazingira
      • Uchumi, Fedha Na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana Na Mwenyekiti
  • Miradi Mbalimbali
    • Progressive projects
    • Itakayo Tekelezwa
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Mkataba wa Huduma Kwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Miongozo
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Machapisho ya Habari
    • Videos
    • Hotuba
    • Makitaba ya Picha
    • Taarifa
    • Matukio
  • Malalamiko

Afya


IDARA  YA  AFYA

MKUU WA  IDARA: DKT BONAVENTURA CHITOPELA


Idara ya Afya ni miongoni mwa idara katika Halmashauri ya Manispaa ya Mji Mafinga. Idara ya Afya inatekeleza majukumu yake kwa kufuata miongozo mbalimbali inayotolewa na Wizara ya afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto. Huduma hizi zimekuwa zikitolewa kwa kushirikiana na wadau mbalimbali kupitia vituo vya kutolea huduma za Afya na kwa njia ya mkoba katika maeneo mbalimbali ya Manispaa. Katika Halmashauri ya  Manispaa ya Mji Mafinga kuna jumla ya vituo 45 vya kutolea huduma za afya. Vituo hivi vinamilikiwa na serikali, watu binafsi, mashirika ya dini pamoja na taasisi za serikali. Vituo vya kutolea huduma za Afya vinavyomilikiwa na serikali ni 15, Vituo 21 vinamilikiwa na watu binafsi, 4 vinamilikiwa na mashirika ya dini na  vituo 5 vinamilikiwa na taasisi za serikali. Kati ya vituo hivyo 45, kuna hospitali 1, vituo vya Afya 12 na zahanati 32.


    MAJUKUMU YA IDARA

Idara ya Afya inatekeleza majukumu makuu mawili abayo ni Afya kinga na Afya tiba.  Kupitia Afya tiba  idara imelenga kutoa matibabu sahihi kwa gharama nafuu kwa wananchi wa Manispaa ya Mji Mafinga pamoja na Wilaya za jirani.  Afya kinga imelenga kuwakinga wananchi wasipate magonjwa yale ya kuambukiza, yasiyoyakuambukiza pamoja na kuzuia magonjwa ya mlipuko kama vile kipindupindu.

    AFYA TIBA

Idara imeendelea kutekeleza majukumu yake kwa kufuata miongozo inayotolewa na Wizara ya Afya, Maendeleo ya jamii, Jinsia, Wazee na Watoto pamoja na kutekeleza mpango mkakati wa afya wa mwaka 2015 -2020. Katika kuhakikisha wananchi wanapata tiba sahihi, idara imekuwa ikitekeleza majukumu yafuatayo:

    Kusimamia manunuzi ya dawa, vitendanishi vya maaabara ,vifaa na vifaa tiba kisha kuvisambaza kwenye vituo vya kutolea huduma za afya.
    Kutoa huduma za matibabu na uuguzi kupitia vituo vya kutolea huduma za Afya zikiwemo huduma za upasuaji mkubwa na mdogo. Huduma hizi ni kwa wagonjwa wa nje na wagonjwa wa kulazwa.
    Kufanya ukaguzi wa dawa na vifaa tiba kwenye vituo vya kutolea huduma za afya
    Kusajili na kuhuisha maduka ya dawa na vipodozi, kuyafanyia ukaguzi mara kwa mara na kuhakikisha yanafuata sheria, kanuni na miongozo inayosimamia uanzishaji na uwepo wa maduka hayo
    Kusimamia pamoja na kuzikagua maabara zote na kuhakikisha zimesajiliwa na zinatoa huduma bora kulingana na miongozo iliyotolewa na Wizara ya Afya.
    Kutoa, kusimamia na kuratibu huduma za afya ya uzazi na mtoto katika Manispaa . Huduma hizi ni pamoja na uzazi salama, huduma za uzazi wa mpango, huduma za chanjo kwa watoto chini ya miaka mitano na akina mama wajawazito, uchunguzi wa saratani ya shingo ya kizazi pamoja na matiti. Huduma nyinginezo ni pamoja na huduma za kuzuia ukatili wa kijinsia na ukatili dhidi ya watoto.
    Kuratibu huduma za kuzuia maambukizi ya Virusi vya Ukimwi na UKIMWI. Huduma zitolewazo ni pamoja na matibabu na matunzo kwa watu wanaoishi na virusi vya UKIMWI, huduma za kuzuia maambukizi toka kwa mama kwenda kwa mtoto, huduma za kuchunguza na kutibu magonjwa ya ngono pamoja na huduma za wagonjwa majumbani. Huduma hizi hutolewa katika vituo vya kutolea huduma za Afya.
    AFYA KINGA
    Idara imeendelea kutekeleza majukumu mbalimbali yanayolenga kuwakinga wananchi na magonjwa ya kuambukiza. Mojukumu hayo ni pamoja na:
    Ukaguzi wa nyumba za kuishi na  majengo ya biashara kama vile nyumba za kulala wageni,majengo ya kutengeneza na kuuza vyakula ili kuondoa machukizo yanayoweza kuhatarisha afya ya binadamu.
       Utoaji wa elimu ya afya kwa umma kuhusu masuala mbalimbali ya afya.
    Utoaji wa chanjo kwa magonjwa ya kuambukiza kwa wajawazito na watoto
    Usimamizi wa afya na usalama mahala pa kazi
    Usimamizi wa usafi wa Mazingira.
    

KITUO CHA AFYA  UPENDO.




UKARABATI WA WODI NAMBA 5 KATIKA HOSPITALI YA MJI MAFINGA

UKARABATI UMEKAMILIKA:

MILIONI 25- KUTOKA SERIKALI KUU

MILIONI 8- MAPATO YA NDANI


JENGO LA KUTOLEA HUDUMA ZA DHARURA(EMD) HOSPITALI YA MJI MAFINGA- LIMEKAMILIKA NA LINATUMIKA



KITUO CHA AFYA BUMILAYINGA- JENGO LA OPD LINATUMIKA- UJENZI MAJENGO MENGINE UNAENDELEA


  • UMUHIMU WA LISHE - FATMA




  •  IRINGA.pdf


DC- MUFINDI DKT. LINDA SALEKWA ATEMBELEA UJENZI WA JENGO LA KUHIFADHIA MAITI LINALOJENGWA KATIKA HOSPITALI YA MJI MAFINGA.


NYUMBA YA WATUMISHI KATIKA ZAHANATI YA KISADA UJENZI UMEGHARIMU KIASI CHA SHILINGI MILIONI 60 KUTOKA MAPATO YA NDANI YA HALMASHAURI YA MJI MAFINGA.


DC MUFINDI MHESHIMIWA DKT LINDA SALEKWA AKIWA NA MKURUGENZI MJI MAFINGA BI, FIDELICA MYOVELLA KWENYE ZIARA YA KUKAGUA MIRADI YA MAENDELEO KATIKA ZAHANATI YA KISADA

UJENZI WA WODI YA DARAJA LA KWANZA KATIKA HOSPITALI YA MJI MAFINGA UNAENDELEA- 

UJENZI WA JENGO LA KUFULIA NGUO UMEKAMILIKA KATIKA KITUO CHA AFYA BUMILAYINGA.



MAPOKEZI YA GARI LA KUBEBA WAGONJWA KATIKA KITUO CHA AFYA IFINGO- LILILOKABIDHIWA KATIKA KITUO HICHO NA MBUNGE WA JIMBO LA MAFINGA MHESHIMIWA COSATO CHUMI

 MKUU WA MKOA WA IRINGA MHESHIMIWA PETER SERUKAMBA AKIKAGUA UJENZI WA JENGO LA KUFULIA NGUO KATIKA HOSPITAL IYA MJI MAFINGA



JENGO LA KUFULIA NGUO KATIKA HOSPITALI YA MJI MAFINGA.


JENGO ,LA KUHIFADHIA MAITI(MOTUARY) KATIKA HOSPITALI YA MJI MAFINGA.

WAZIRI MKUU WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA MHESHIMIWA KASSIM MAJALIWA MAJALIWA(MB) ALIPOTEMBELEA  NA KUKAGUA MAJENGO KATIKA HOSPITALI YA MJI MAFINGA 2024.



                              UJENZI WA JENGO LA HUDUMA ZA MAMA NA MTOTO KATIKA HOSPITALI YA MJI MAFINGA UNAENDELEA


                                                                                     JENGO LA ICU KATIKA HOSPITALI YA MJI MAFINGA 



Matangazo

  • NAFASI ZA MASOMO KWA SHULE YA CHIEF MKWAWA ENGLISH MEDIUM- HALMASHAURI YA MJI MAFINGA. NAFASI BADO ZIPO TUPIGIE January 29, 2024
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA YANAPATIKANA www.mafingatc.go.tz July 13, 2024
  • MJI MAFINGA YAVUKA LENGO UKUSANYAJI MAPATO YAKUSANYA ASILIMIA 113 KWA MWAKA WA FEDHA 2023/2024 August 14, 2024
  • MATOKEO YA DARASAM LA SABA 2024 YANAPATIKANA KWENYE TOVUTI YETU .www.mafingatc.go.tz October 30, 2024
  • View All

Habari mpya

  • MASHINDANO YA UMISSETA NA UMITASHUMTA KUKUZA FURSA ZA UCHUMI NA UTALII IRINGA

    June 09, 2025
  • UMISSETA NA UMITASHUMTA KUANZA KUTIMUA VUMBI IRINGA

    June 09, 2025
  • KAIMU MKURUGENZI NDUGU CHARLES MWAITEGE AMEENDESHA KIKAO CHA KAMATI YA LISHE ROBO YA TATU

    June 06, 2025
  • MADAKTARI BINGWA KUTOA HUDUMA HOSPITALI YA MJI MAFINGA

    June 03, 2025
  • View All

Video

SENSA NI MAENDELEO
Video zaidi

Viungo Vya Haraka

  • Maelezo na Form Ya kiapo cha uadilifu
  • https://matokeo.necta.go.tz
  • Muongozo wa matumizi ya TEHAMA serikalini

Tovuti Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya wananchi

Watembeleaji kidunia

world map hits counter

Idadi ya watu wanao tembelea Tovuti

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana na sisi

    Mafinga Town.

    Postal Address: Po.Box 76 Mafinga

    Simu: +255 262 772 393

    Mobile: 026-2772393

    Barua Pepe: td@mafingatc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Disclamer
    • Maswali
    • Sitemap
    • Huduma

Copyright ©2018 Mafinga Town Council . All rights reserved.