Benki ya Mucoba Mafinga wamekabidhi mapipa 4 ya kutunzia taka kwa Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Mafinga Ndugu, Charles Karibu Tuyi ambaye amemwakilisha Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Mafinga katika kuadhimisha Wiki ya Huduma kwa Wateja ambapo Wiki ya Huduma kwa Wateja Benki ya Mucoba Mafinga imejikita katika suala la Mazingira katika kuwezesha kutoa huduma safi na salama kwa Wateja.
Akizungumza Meneja wa Benki ya Mucoba Mafinga Ndugu , Phillipo Fanuel Raymond amesema uzinduzi wa Wiki ya Huduma kwa Wateja Benki ya Mucoba Mafinga imejikita katika kutoa semina ya usafi wa mazingira lengo kuu ni kuhakikisha Wateja wa Benki ya Mucoba Mafinga wanaishi katika mazingira safi na salama tunaimani kwa kufanya hivo tutakuwa na Wateja wazuri.
Naye Mkuu wa Kitengo cha Masoko Benki ya Mucoba Mafinga Amina Abdi Mikongomi amesema Benki ya Mucoba Mafinga katika kuadhimisha Wiki ya Huduma kwa Wateja wamekwenda mbali zaidi kwa kuweza kutoa huduma ya uwekaji akiba na mikopo kwa Wateja ambapo Benki ya Mucoba Mafinga katika kuadhimisha Wiki ya Huduma kwa Wateja kipaumbele chake ni kwetu sisi jamii kwanza tupo tayari kukusikiliza.
Aidha Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Mafinga Ndugu, Charles Karibu Tuyi ambaye ni Mkuu wa Idara ya Mazingira amewashukuru Benki ya Mucoba Mafinga kwa kuweza kuwapatia Mapipa 4 ya kutunzia taka amesema Halmashauri ya Mji Mafinga imepokea vitendea kazi hivo kwani kwa kufanya hivo wanatimiza mujibu wa sheria ya Mazingira namba 20 ya Mwaka 2004 ambayo inasema kila binadamu anayo haki ya kuishi mazingira safi na salama na walichokifanya ni kurudisha kwa jamii katika kuwaweka Wateja wao mahali safi na salama.
IMETOLEWA NA KITENGO CHA MAWASILIANO SERIKALINI MAFINGA TC
Christopher Mhina
Mwandishi wa Habari Mafinga TC
Mafinga Town.
Postal Address: Po.Box 76 Mafinga
Simu: +255 262 772 393
Mobile: 026-2772393
Barua Pepe: td@mafingatc.go.tz
Copyright ©2018 Mafinga Town Council . All rights reserved.