Halmashauri ya Mji Mafinga imepokea vikombe 7 kwenye mashindano ya Umoja wa Michezo na Taaluma kwa wanafunzi wa Shule za Sekondari(UMISSETA)
ngazi ya Mkoa yaliyofanyika Shule ya Sekondari JJ Mungai mjini Mafinga kuanzia tarehe 5/6/2023-mpaka tarehe 6/6/2023 na kushirikisha Halmashauri zote 5 katika Mkoa wa Iringa.
Akizungumza Mkuu wa Kitengo cha Utamaduni, Sanaa na Michezo Halmashauri ya Mji Mafinga Ndg. Henry Kapella amesema kuwa vikombe ambavyo vimechukuliwa na Halmashauri ya Mji Mafinga ni katika michezo :-Ngoma
Mshindi 1
Mpira wa wavu ke- Mshindi 1
Mpira wa Miguu me-Mshindi 2
Mpira wa mkono me- Mshindi 2
Usafi- Mshindi 1
Mpira wa pete- Mshindi wa 2
Mpira wa Meza me- Mshindi wa 2
Na zaidi Halmashauri imefanikiwa kuingiza wana michezo wanafunzi 15 Kati ya wanafunzi 80 wanaounda timu ya UMISSETA mkoa.
Akizungumza Mwenyekiti wa Wakuu wa Shule Mkoa wa Iringa(TAOSA) Ndugu, Albert Mkollo amesema Michezo inaweza kuchochochea Uchumi na mapato ya Eneo husika hivyo, ameomba walimu na wataalamu wa Halmashauri kuipa kipaumbele michezo kwani inaongeza mapato ya Halmashauri na kujenga afya ya akili ya mwanafunzi.
Afisa Elimu Sekondari Mwalimu Stephen Shemdoe amesema Halmashauri imeandaa mafunzo kwa walimu Hasa wa michezo ya basketball kwa mwakani na kutenga Bajeti ya michezo ya UMISSETA kupitia mapato ya ndani. Hivyo Halmashauri imeandaa mikakati hiyo kwa kuzingatia umuhimu wa michezo kwa Halmashauri ya Mji Mafinga.
Nae Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Mafinga ndugu Apolinary Seiya akipokea vikombe 7 vya ushindi ametoa Pongezi kwa walimu wa michezo, Afisa Elimu Sekondari , wakuu wa Shule kwa michango yao na chakula kwaajili ya wanafunzi walioko kambi.
Amesema imetengwa Bajeti kwa mwaka ujao kwaajili ya kuchangia michezo na miundombinu ya michezo.
Aidha amewaasa walimu wanaoeda Tabors kuhakikisha wanadumisha nidhamu na kucheza kwa bidii ili kurudi na ushindi.
IMEANDALIWA NA KITENGO CHA MAWASILIANO SERIKALINI - MAFINGA TC
Sima Bingileki
Mkuu wa Kitengo Cha Mawasiliano Serikalini- Mafinga TC
Mafinga Town.
Postal Address: Po.Box 76 Mafinga
Simu: +255 262 772 393
Mobile: 026-2772393
Barua Pepe: td@mafingatc.go.tz
Copyright ©2018 Mafinga Town Council . All rights reserved.