Lengo la Maonesho haya ni kutangaza vivutio vya Utalii na maeneo ya uwekezaji nyanda za Juu Kusini.
Halmashauri ya Mji Mafinga ina maeneo makubwa ya uwekezaji wa viwanda na maeneo ya Utalii, kama mapango, kaburi la Mwinyigumba ambaye alikuwa baba yake Mkwawa, vyungu, mawe ya zamani ya kunolea visu na miti mikubwa ya kijani ya asili katika shamba la miti Saohill.
Akizungumza Mkurugenzi wa Mji Mafinga Ndugu, Ayoub Kambi amesema kitengo cha Biashara na Uwekezaji kimejipanga kuhakikisha kuwa mwekezaji anapofika Halmashauri ya Mji Mafinga anapata huduma stahili kwa haraka ili aweze kuwekeza kwani kwa kufanya hivyo mapato ya nchi yanaongezeka na watanzania wanapata ajira.
Aidha amewakaribisha watanzania kufanya utalii wa ndani na kujionea vitu mbalimbali vinavyopatikana Mji mafinga kama machimbo ya udongo mweupe unautumika kutengeneza unga wa jipsum pamoja na kaburi la Mwinyigumba.
Maonesho ya Karibu Kusini 2023 yanayoendelea katika viwanja vya Kihesa Kilolo yalizinduliwa tarehe 23/9/2023 na Waziri wa Maliasili na Utalii, Mheshimiwa Angellah Kairuki(MB) ambapo Mikoa 10 imeratibu Maonesho hayo ya Utalii Karibu Kusini na waoneshaji zaidi ya 130 wameshiriki.
Sima Bingileki
Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini- Mafinga TC
Mafinga Town.
Postal Address: Po.Box 76 Mafinga
Simu: +255 262 772 393
Mobile: 026-2772393
Barua Pepe: td@mafingatc.go.tz
Copyright ©2018 Mafinga Town Council . All rights reserved.