• Malalamiko |
    • Wasiliana na sisi |
    • Maswali |
    • Baruapepe |
Mafinga Town Council
Mafinga Town Council

Jamhuri Ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Mafinga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Organization Structure
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Kilimo na umwagiliaji
      • Fedha
      • Mipango na Takwimu
      • Elimu ya Sekondari
      • Elimu ya Msingi
      • Afya
      • Ardhi na Maliasili
      • Community Development,Social welfare Gender and Youth
      • Water
      • Work
    • Vitengo
      • Community
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Huduma za Kisheria
      • Biashara
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa madiwani
    • Kamati Za Kudumu Za Halmashauri
      • Fedha Na uongozi
      • Mipangomiji Namazingira
      • Uchumi, Fedha Na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana Na Mwenyekiti
  • Miradi Mbalimbali
    • Progressive projects
    • Itakayo Tekelezwa
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Mkataba wa Huduma Kwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Miongozo
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Machapisho ya Habari
    • Videos
    • Hotuba
    • Makitaba ya Picha
    • Taarifa
    • Matukio
  • Malalamiko

HALMASHAURI YA MJI MAFINGA YAPOKEA PIKIPIKI KUTOKA PANDAMITI KIBIASHARA KWAAJILI YA KUBORESHA SEKTA YA MISITU

Posted on: December 1st, 2022

HALMASHAURI YA MJI MAFINGA YAPOKEA PIKIPIKI KWAAJILI YA KUBORESHA SEKTA YA MISITU

Jumla ya pikipiki 12 zenye thamani ya shilingi Milioni 120 zimetolewa na Panda Miti Kibiashara kwaajili ya kuboresha huduma za Ugani ikiwemo kufanya doria kwenye mashamba, kutoa taarifa za moto, kutunza vyanzo vya maji na kudhibiti moto katika Halmashauri 10 zinazofanya kazi na Mradi huu Tanzania.

Akizungumza Mkuu wa Wilaya ya Mufindi Mheshimiwa Saad Mtambule amepokea pikipiki 3 kwaajili ya Halmashauri ya Mji Mafinga, Halmashauri ya Mufindi na Halmashauri ya Wilaya ya Kilolo kwa niaba.Amesema Mazao yatokanayo na Misitu ni moja ya kianzia kikubwa cha Mapato kwa Halmashauri za Mafinga Mji na Halmashauri ya Mufindi.

“ Sekta ya Misitu inatupa sana faida, lakini changamoto kubwa ni namna ya kupanda miti na kudhibiti uchomaji wa moto, jambo ambalo linarudisha nyuma maendeleo ya nchi na kushusha mapato ya Halmashauri. Hivyo elimu izidi kutolewa kuhusu upandaji wa miti wa kitaalamu na madhara ya moto “.

Akizungumza Mshauri wa Kiufundi wa Mpango Bwana Michael  Hawkes amesema kuwa Mpango umesaidia kuongeza uzalishahi bora wa miti kwa wakulima waliopata mafunzo  na kugundua viashiria vya moto na namna ya kujikinga na moto. Amesema Mradi wa Panda Miti Kibiashara awamu ya pili umetekelezwa kwenye Halmashauri 10 na wananchi wamepewa elimu mbalimbali ambayo hata mradi ukiisha Mwezi wa 10/ 2023 wananchi wataendelea kuitumia elimu hiyo kwa vizazi vijavyo na Uchumi Endelevu.

Katika hafla hiyo Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Mafinga Bi Happiness Laizer amemuhakikishia Mkuu wa Wilaya na Uongozi wa Panda Miti Kibiashara kuwa Chombo hicho kitatunzwa na kutumika kwenye kazi kusudiwa tu hasa Doria  kwenye sekta ya mazao ya misitu.


Akipokea pikipiki hiyo yenye namba za usajili  DFP 9187 Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji Mafinga Mheshimiwa Regnant Kivinge amesema kuwa kwa Halmashauri ya Mji Mafinga mradi wa PandaMiti Kibiashara umesaidia vijana wengi kupata taaluma ya kupanda miti hasa ukizingatia kuwa moja ya uchumi mkubwa wa wananchi wa Mafinga ni mazao ya misitu.

Akithibitisha umuhimu wa chombo hicho Mratibu wa Panda Miti Kibiashara upande wa Mji Mafinga Bwana Demitrus Kamtoni amesema kuwa uwepo wa pikipiki hiyo utasaidia kuboresha huduma za ugani kwenye mazao ya misitu ikiwemo kufanya doria kutoa Elimu mara kwa mara ya madhara ya moto, kulinda vyanzo vya maji na kudhibiti wizi wa mazao ya misitu.

Mratibu wa PandaMiti Kibiashara Awamu ya tatu Mafinga Bwana Nyachia Roberts amesema kuwa Mradi huu umetekelezwa kwa muda wa miaka minne na utakamilika mwezi wa Oktoba 2023 ambapo umetekekezwa katika Halmashauri 10 , kwa mkoa wa Iringa Mradi unatekelezwa katika Halmashauri ya Mji Mafinga, Mufindi na Kilolo. Aidha mradi umekabidhi vifaa vya kukata matawi ya miti(misumeno 97)kwa kila Halmashauri.

IMEANDALIWA NA KITENGO CHA MAWASILIANO SERIKALINI- MAFINGA TC

Sima Bingileki

Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini- MafingaTc

Matangazo

  • NAFASI ZA MASOMO KWA SHULE YA CHIEF MKWAWA ENGLISH MEDIUM- HALMASHAURI YA MJI MAFINGA. NAFASI BADO ZIPO TUPIGIE January 29, 2024
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA YANAPATIKANA www.mafingatc.go.tz July 13, 2024
  • MJI MAFINGA YAVUKA LENGO UKUSANYAJI MAPATO YAKUSANYA ASILIMIA 113 KWA MWAKA WA FEDHA 2023/2024 August 14, 2024
  • MATOKEO YA DARASAM LA SABA 2024 YANAPATIKANA KWENYE TOVUTI YETU .www.mafingatc.go.tz October 30, 2024
  • View All

Habari mpya

  • TUME HURU YA TAIFA YA UCHAGUZI IMEENDESHA MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA KWA AWAMU YA PILI JIMBO LA MAFINGA MJINI

    May 02, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 KATIKA HALMASHAURI YA MJI MAFINGA UMEPITIA JUMLA YA MIRADI 11 YA MAENDELEO YENYE THAMANI YA SHILINGI BILIONI 3.1

    May 01, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 KATIKA HALMASHAURI YA MJI MAFINGA UMEPITIA JUMLA YA MIRADI 11 YA MAENDELEO YENYE THAMANI YA SHILINGI BILIONI 3.1

    May 01, 2025
  • MBUNGE WA MAFINGA MJI AKABIDHI MITUNGI YA GESI

    May 01, 2025
  • View All

Video

SENSA NI MAENDELEO
Video zaidi

Viungo Vya Haraka

  • Maelezo na Form Ya kiapo cha uadilifu
  • https://matokeo.necta.go.tz
  • Muongozo wa matumizi ya TEHAMA serikalini

Tovuti Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya wananchi

Watembeleaji kidunia

world map hits counter

Idadi ya watu wanao tembelea Tovuti

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana na sisi

    Mafinga Town.

    Postal Address: Po.Box 76 Mafinga

    Simu: +255 262 772 393

    Mobile: 026-2772393

    Barua Pepe: td@mafingatc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Disclamer
    • Maswali
    • Sitemap
    • Huduma

Copyright ©2018 Mafinga Town Council . All rights reserved.