Jumla ya Miche 330 ya parachichi imepandwa katika Shule ya Sekondari ya JJ Mungai na Changarawe ikiwa ni kusherehekea maadhimisho ya Miaka 59 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar .
Akizungumza Afisa Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira Ndugu, Demitrus Kamtoni amesema kuwa lengo kusudiwa ni kupanda miche 1,500,000 kwa Halmashauri ambapo mpaka sasa miche 1,721,402 imeshapandwa na kuvuka lengo katika maeneo mbalimbali Halmashauri ya Mji kwa kusudi la kuhifadhi Mazingira, kuongeza lishe kuleta kivuli na kupambana na Tabia nchi .
Amesema kila Shule inatakiwa ipande miche ya miti ya matunda isiyopungua 10 kulingana na ukubwa wa eneo lao na zoezi linaendelea katika Shule mbalimbali.
Maadhimisho ya Miaka 59 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar yanaadhimishwa kila tarehe 26/4 ambapo kwa Mwaka huu Halmashauri ya Mji Mafinga imeadhimisha miaka 59 ya Muungano kwa kupanda miti na kushiriki michezo kimkoa kwa timu za mpira wa pete na mpira wa miguu.
“MIAKA 59 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar
Umoja na Mshikamano ndiyo nguzo ya kukuza Uchumi wetu.”
IMEANDALIWA NA KITENGO CHA MAWASILIANO SERIKALINI- MAFINGA TC
Sima Bingileki
Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini-Mafinga TC
Angela Kairuki
Ofisi ya Rais - Tamisemi
Halima DendegoMaelezo News
CCM TANZANIA
Mafinga Town.
Postal Address: Po.Box 76 Mafinga
Simu: +255 262 772 393
Mobile: 026-2772393
Barua Pepe: td@mafingatc.go.tz
Copyright ©2018 Mafinga Town Council . All rights reserved.