MAFINGA TC YAKABIDHI MADARASA 10 YA KIDATO CHA KWANZA -2023 KWA RC IRINGA.
Mkuu wa Wilaya ya Mufindi Mheshimiwa Saad Mtambule kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa Mheshimiwa Halima Dendego amepokea madarasa kumi kutoka kwa Halmashauri ya Mji Mafinga yaliyokamilika yenye thamani ya shilingi milioni 200 fedha kutoka Serikali Kuu kwaajili ya Wanafunzi wa kidato cha Kwanza 2023.
Akipokea madarasa hayo Mkuu wa Wilaya ya Mufindi Amesema Serikali imejitahidi kuleta fedha kwaajili ya ujenzi wa madarasa ili wanafunzi waweze kusoma kwenye Mazingira bora ili kuboresha hali ya ufaulu na Mazingira mazuri ya kusomea hivyo walimu wahakikishe ufaulu wa Shule na Matokeo yanaendana na ubora wa majengo.
“ walimu hakikisheni ubora wa Shule unaendana na matokeo mazuri ya Shule hatutaki ziro, hakikisheni ufaulu unaongezeka na nidhamu ya walimu na wanafunzi Ndio Inaleta matokeo chanya kwani kukiwa na nidhamu kila mtu atatimiza wajibu Wake” Saad Mtambule Dc Mufindi.
Akizungumza kwenye hafla hiyo ya Makabidhiano, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Iringa ACP Allan Bukumbi amesema kuwa Ushirikiano mkubwa ambao umeonyeshwa na wana mafinga kati ya walimu, uongozi wa Chama Cha Mapinduzi na watumishi wa Halmashauri ndio Matokeo ya Ujenzi huu mzuri wa madarasa. Matumizi ya fedha na ubora wa majengo unaendana hakika tunawapongeza.
Nae Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Mufindi Mheshimiwa George Kavinuke amesema kuwa Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dr.Samia Suluhu Hassan amesema kuwa Serikali ya Awamu ya sita imekuwa ikileta mabilioni ya fedha kwenye Halmashauri ikiwa ni kuboresha Miundo Mbinu ya Shule, hivyo kama Halmashauri tuhakikishe tunatenga bajeti kwaajili ya kuboresha madarasa yaliyochakaa kwenye shule hizo ili kusaidia kuunga mkono juhudi za Serikali za kuhakikisha wanafunzi wanasomea katika mazingira bora.
Jumla ya madarasa 10 ya kidato cha kwanza 2023 yamekamilika na kukabidhi kwa Mkuu wa Mkoa wa Iringa . Halmashauri ya Mji
Mafinga ilipokea kiasi cha Shilingi milioni 200 kutoka Serikali Kuu mwezi wa Kumi 2022 kwaajili ya Ujenzi wa madarasa kumi ambapo Bumilayinga Sekondari walipokea kiasi cha Shilingi milioni 40 Ujenzi wa madarasa 2, Isalavanu Sekondari madarasa 2 shilingi milioni 40, Ihongole Sekondari darasa 1,Shilingi milioni 20,Upendo Sekondari madarasa 3, walipokea milioni 60 na Luganga sekondari darasa 1 milioni 20.
Hafla ya makabidhiano imehudhuriwa na Kamati yq Ulinzi ya Mkoa, Kamati ya Ulinzi wilaya, Mwenezi Wilaya ya Mufindi, viongozi mbalimbali wa Chama Cha Mapinduzi(CCM) waheshimiwa madiwani wananchi na watumishi wa Halmashauri ya Mji Mafinga wakiongozwa Kaimu Mkurugenzi Mwalimu Doroth Kobelo
IMEANDALIWA NA KITENGO CHA MAWASILIANO MAFINGA TC
Sima Bingileki
Kaimu Mkuu wa Kitengo Cha Mawasiliano Serikalini- Mafinga TC
Mafinga Town.
Postal Address: Po.Box 76 Mafinga
Simu: +255 262 772 393
Mobile: 026-2772393
Barua Pepe: td@mafingatc.go.tz
Copyright ©2018 Mafinga Town Council . All rights reserved.