Mkuu wa Mkoa wa iringa Mhe Queen Sendiga amekabidhiwa madarasa 16 ya mpango maendeleo ya ustawi wa taifa na mapambano dhidi ya UVIKO 19 larehe 16/12/2021.Akikabidhi madarasa hayo katika hafla iliyofanyika katika shule ya sekondari ya J J Mungai Mkuu wa wilaya ya Mufindi Mhe Saad Mtambule alipongeza sana uongozi wa halmashauri ya mji Mafinga kwa usimamizi mzuri wa kazi na yenye kiwango bora sana.Mkuu wa mkoa wakati wa ziara yake ya ukaguzi wa madarasa iliyofanyika kwa kupitia shule za sekondari za kinyanambo,isalkavanu,changarawe na hatimaye JJ Mungai alipongeza sana halmashauri ya mji kwa kuwa ya kwanza kumaliza kazi ya ujenzi na kwa kiwango kikubwa.Akiongea na wananchi pamoja na viongozi wa chama na serikali baada ya kupanda mti wa kumbukumbu wa kuonyesha kuridhishwa na ujenzi aliwasisitiza kuendelea kufanya kazi kwa ushirikiano
Mafinga Town.
Postal Address: Po.Box 76 Mafinga
Simu: +255 262 772 393
Mobile: 026-2772393
Barua Pepe: td@mafingatc.go.tz
Copyright ©2018 Mafinga Town Council . All rights reserved.