• Malalamiko |
    • Wasiliana na sisi |
    • Maswali |
    • Baruapepe |
Mafinga Town Council
Mafinga Town Council

Jamhuri Ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Mafinga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Organization Structure
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Kilimo na umwagiliaji
      • Fedha
      • Mipango na Takwimu
      • Elimu ya Sekondari
      • Elimu ya Msingi
      • Afya
      • Ardhi na Maliasili
      • Community Development,Social welfare Gender and Youth
      • Water
      • Work
    • Vitengo
      • Community
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Huduma za Kisheria
      • Biashara
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa madiwani
    • Kamati Za Kudumu Za Halmashauri
      • Fedha Na uongozi
      • Mipangomiji Namazingira
      • Uchumi, Fedha Na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana Na Mwenyekiti
  • Miradi Mbalimbali
    • Progressive projects
    • Itakayo Tekelezwa
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Mkataba wa Huduma Kwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Miongozo
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Machapisho ya Habari
    • Videos
    • Hotuba
    • Makitaba ya Picha
    • Taarifa
    • Matukio
  • Malalamiko

VIPIGO MAJERAHA MENGI KWA WATOTO YANASABABISHWA NA WAKINA MAMA MAJUMBANI- HUO NI UKATILI WA KIJINSIA

Posted on: June 17th, 2022

VIPIGO NA MAJERAHA MENGI KWA WATOTO YANASABABISHWA NA WAKINA MAMA- HUO NI UKATILI WA KIJINSIA.

Mkuu wa Mkoa wa Iringa Mheshimiwa Queen Sendiga amesema vipigo na majeraha mengi kwa watoto vinatoka kwa akina mama, walezi au wazazi. Tuache huo ni ukatili wa kijinsia.

“Wazazi walezi tumewasogenza  pembeni watoto katika jukumu la kuwalea na kuwatunza, ni jukumu letu sote tunatakiwa kuwalinda na kuwakumbatia watoto wetu.”

Mkuu wa Mkoa ameyasema hayo kwenye maadhimisho ya Siku ya Mtoto wa Afrika ambapo kwa Mkoa wa Iringa Maadhimisho yamefanyika Katika Mji wa Mafinga Shule ya Msingi Makalala.

Amesema kuwa wazazi wengi wamekuwa wakiwatuma watoto katika kutafuta chakula cha familia huku wao wakiwa vilabuni, hii sio sawa kabisa na mzazi atakayekutwa kamtuma mtoto kuuza bidhaa kwaajili ya kulisha familia atachukuliwa hatua kali. Jukumu la watoto ni kusoma, kutunzwa na kupendwa.

“Kuna wazazi wengine wanaenda kwenye shughuli zao na kuacha watoto wakileana nyumbani, unakuta mtoto mdogo wa miaka 10 anawalea wenzake wawili, ni majukumu makubwa tuache wazazi kwani huu pia ni ukatili wa kijinsia.”

Akisoma risala kwa Mgeni rasmi Mtoto Peter Sinkala wa Shule ya Msingi Makalala amesema Watoto wanaomba serikali iwasaidie watoto wote wenye ulemavu tofauti tofauti kupewa vifaa kwaajili ya kusomea na wale watoto wenye uwezo lakini ni walemavu waliofichwa majumbani wapelekwe shule.

Amesema watoto wote ni sawa wa kike na kiume hivyo wasibaguliwe katika kupata haki zao hasa kwenye ngazi za familia, watoto waachwe wasome hasa wa kike ili kuja kutimiza ndoto zao wasikatishwe masomo.

Maadhimisho ya Mtoto wa Afrika yamehudhuriwa na Viongozi mbalimbali wa Chama na Serikali ngazi ya Mkoa, viongozi wa Wilaya ya Mufindi akiwemo Mkuu wa Wilaya ya Mufindi Mheshimiwa Saad Mtambule, Mkurugenzi wa Mji Mafinga Bi, Happiness Laizer pamoja na wananchi wa Halmashauri ya Mji wa Mafinga.


IMEANDALIWA NA OFISI YA HABARI NA MAWASILIANO

SIMA BINGILEKI

AFISA HABARI MKUU

Matangazo

  • NAFASI ZA MASOMO KWA SHULE YA CHIEF MKWAWA ENGLISH MEDIUM- HALMASHAURI YA MJI MAFINGA. NAFASI BADO ZIPO TUPIGIE January 29, 2024
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA YANAPATIKANA www.mafingatc.go.tz July 13, 2024
  • MJI MAFINGA YAVUKA LENGO UKUSANYAJI MAPATO YAKUSANYA ASILIMIA 113 KWA MWAKA WA FEDHA 2023/2024 August 14, 2024
  • MATOKEO YA DARASAM LA SABA 2024 YANAPATIKANA KWENYE TOVUTI YETU .www.mafingatc.go.tz October 30, 2024
  • View All

Habari mpya

  • TUME HURU YA TAIFA YA UCHAGUZI IMEENDESHA MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA KWA AWAMU YA PILI JIMBO LA MAFINGA MJINI

    May 02, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 KATIKA HALMASHAURI YA MJI MAFINGA UMEPITIA JUMLA YA MIRADI 11 YA MAENDELEO YENYE THAMANI YA SHILINGI BILIONI 3.1

    May 01, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 KATIKA HALMASHAURI YA MJI MAFINGA UMEPITIA JUMLA YA MIRADI 11 YA MAENDELEO YENYE THAMANI YA SHILINGI BILIONI 3.1

    May 01, 2025
  • MBUNGE WA MAFINGA MJI AKABIDHI MITUNGI YA GESI

    May 01, 2025
  • View All

Video

SENSA NI MAENDELEO
Video zaidi

Viungo Vya Haraka

  • Maelezo na Form Ya kiapo cha uadilifu
  • https://matokeo.necta.go.tz
  • Muongozo wa matumizi ya TEHAMA serikalini

Tovuti Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya wananchi

Watembeleaji kidunia

world map hits counter

Idadi ya watu wanao tembelea Tovuti

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana na sisi

    Mafinga Town.

    Postal Address: Po.Box 76 Mafinga

    Simu: +255 262 772 393

    Mobile: 026-2772393

    Barua Pepe: td@mafingatc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Disclamer
    • Maswali
    • Sitemap
    • Huduma

Copyright ©2018 Mafinga Town Council . All rights reserved.