WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema Tanzania ni miongoni mwa nchi zinazofanya kazi kwa karibu sana na sekta binafsi ili kukuza uchumi na kuleta maendeleo kwa wananchi wake.
Ametoa kauli hiyo jana jioni (Jumatatu, Mei 12, 2025) wakati akishiriki mjadala uliojumuisha mawaziri wakuu wanne kutoka Tanzania, Ivory Coast, Guinea na Cameroun katika moja ya vikao vya jukwaa la siku mbili la Maafisa Watendaji Wakuu barani Afrika ambao unaendelea hoteli ya Sofitel jijini Abidjan, Ivory Coast.
Waziri Mkuu Majaliwa ambaye anamwakilisha Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan katika jukwaa hilo alitumia fursa hiyo kuelezea namna ambavyo Serikali ya Tanzania imekuwa ikiishirikisha sekta binafsi kwa kufungua milango ya fursa mbalimbali ili iweze kutumika na kuleta manufaa katika nchi.
“Serikali ya Tanzania inafanya kazi kwa karibu na Tanzania Private Sector Foundation, vyama vya wafanyakazi, vya waajiri na wenye viwanda na pia inawapa fursa ya kujenga mshikamano kwa kufanya kazi na Serikali. Pia imefungua milango kwa wawekezaji kutoka ndani ya nchi, nje ya bara la Afrika na duniani kwa ujumla ili kukuza uchumi wa ndani.”
Waziri Mkuu ametumia fursa hiyo kuwaeleza faida za African Continental Free Trade Area (AfCFTA) na jinsi ambavyo Tanzania imetumia fursa hiyo kuimarisha miundombinu ya reli na bandari kutokana na nafasi yake kijiografia. “Tumeimarisha bandari za Tanga, Dar es Salaam na Mtwara na pia tuna mpango wa kuanza ujenzi wa bandari ya Bagamoyo,” alisema.
Amesema Tanzania inaendelea na ujenzi wa reli ya kisasa ya SGR ili kuziunganisha nchi za Congo, Rwanda na Burundi, pia kuna reli ya TAZARA inayokwenda Zambia. Tumeimarisha usafiri wa anga na barabara ili kuwawezesha wanaokuja kuwekeza Tanzania wapate urahisi wa huduma muhimu.
Mafinga Town.
Postal Address: Po.Box 76 Mafinga
Simu: +255 262 772 393
Mobile: 026-2772393
Barua Pepe: td@mafingatc.go.tz
Copyright ©2018 Mafinga Town Council . All rights reserved.