• Malalamiko |
    • Wasiliana na sisi |
    • Maswali |
    • Baruapepe |
Mafinga Town Council
Mafinga Town Council

Jamhuri Ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Mafinga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Organization Structure
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Kilimo na umwagiliaji
      • Fedha
      • Mipango na Takwimu
      • Elimu ya Sekondari
      • Elimu ya Msingi
      • Afya
      • Ardhi na Maliasili
      • Community Development,Social welfare Gender and Youth
      • Water
      • Work
    • Vitengo
      • Community
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Huduma za Kisheria
      • Biashara
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa madiwani
    • Kamati Za Kudumu Za Halmashauri
      • Fedha Na uongozi
      • Mipangomiji Namazingira
      • Uchumi, Fedha Na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana Na Mwenyekiti
  • Miradi Mbalimbali
    • Progressive projects
    • Itakayo Tekelezwa
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Mkataba wa Huduma Kwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Miongozo
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Machapisho ya Habari
    • Videos
    • Hotuba
    • Makitaba ya Picha
    • Taarifa
    • Matukio
  • Malalamiko

Zaidi ya Bilioni 25 .2 za Bajeti ya 2019/2020 zapitishwa na Baraza la Madiwani Halmashauri Mji Mafinga.

Posted on: February 18th, 2019

Mkutano maalumu wa baraza la madiwani la Halmashauri ya Mji Mafinga limepitisha rasimu ya mpango wa bajeti ya kipindi cha mwaka wa fedha 2019/2020 na kuidhinisha kukusanya na kutumia zaidi ya Bilioni 25.2 kwa ajili ya matumizi ya mishahara, mengineyo na miradi ya maendeleo.

Akisoma rasimu hiyo kwa niaba ya Mkurugenzi, Afisa Mipango wa Halmashauri ya Mji Mafinga Bwana Andambike Kyomo amesema zaidi ya Bilioni 3.9 zinakadiriwa kukusanywa kutokana na vyanzo mbalimbali vya mapato ndani ya Halmashauri.

Makisio hayo ni zaidi ya milioni 648.8 ambayo ni asilimia 20% ukilinganisha na makisio ya mwaka 2018/2019 ya zaidi ya Tsh bilioni 3.3, aidha katika mapato hayo kiasi cha zaidi ya Tsh milioni 602.8 ni mapato ya vyanzo fungiwa katika idara ya afya na elimu sekondari hivyo kufikia mapato halisi kuwa zaidi ya bilioni 3.3.

Baraza hilo limeridhia pia matumizi ya kawaida kwa mwaka wa fedha 2019/2020 ambapo zaidi ya bilioni 17.8 zimeidhinishwa kwa ajili ya matumizi ya kawaida na mishahara , kati ya fedha hizo kiasi cha zaidi ya Tsh bilioni 13.8 ni kwa ajili ya mishahara, na zaidi ya bilioni 4 ni kwa ajili ya matumizi mengineyo.

Aidha baraza hilo limeidhinisha pia kukusanya na kutumia zaidi ya bilioni 7.3 kwa ajili ya kutekeleza miradi ya maendeleo kutoka vyanzo mbalimbali vya mapato kati ya fedha hizo zaidi ya bilioni 4.7 ni kutoka ruzuku ya Serikali kuu, wahisani zaidi ya milioni 490, Halmashauri inatarajia kuchangia zaidi ya bilioni 1.3 sawa na asilimia 40 ya mapato halisi ya ndani ya Halmashauri na nguvu ya wananchi wanatarajia kuchangia zaidi ya milioni 768.

Akieleza matarajio ya utekelezaji wa rasimu ya bajeti hiyo ya 2019/2020 Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Mafinga Bwana Voster Mgina ametanabaisha kwamba bajeti hiyo italenga kuimarisha mifumo ya ukusanyaji na kuongeza mapato ya ndani, kuongeza viwanda na fursa za uwekezaji, kuboresha huduma za usafi katika mji, kuboresha makazi na mipango miji sanjari na kuboresha mazingira ya kufanyia kazi na vitendea kazi na hatimae kukamilisha miradi viporo iliyoanzishwa siku nyingi katika sekta ya afya, elimu utawala na ujenzi.

Akiongoza baraza hilo Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji Mafinga Mhe. Charles Makoga amewahakikishia wananchi wa Mafinga kwamba bajeti hiyo iliyoidhinishwa leo hii itaenda kutekelezwa ipasavyo na imelenga kutatua kero za wananchi.

“Sisi kama watekelezaji wa ilani ya chama cha mapinduzi wote kwa pamoja kwa kushirikiana na madiwani wa chadema kwa pamoja tunashirikiana kuhakikisha bajeti hii inaenda kutekelezwa katika kata zetu zote kama iliyopangwa bila kujali vyama vyetu kwani maendeleo hayana chama” Alisema

Aidha ameeleza kwamba katika kuendelea kuunga mkono juhudi za Mhe. Rais Dkt John Magufuli za kuleta elimu bure na matokeo chanya yanayotokea ya ongezeko la wanafunzi, Halmashauri yake imejiandaa kuongeza kujenga shule mbili za Sekondari mpya ikiwemo ya vipaji maalumu na nyingine ya Wasichana itakayojulikana kwa jina la Mafinga Girls hii ni kutokana na ongezeko la ufaulu wa mtihani wa darasa la saba ambapo halmashauri hiyo imefikia asilimia 92.86% ya ufaulu kwa mwaka 2018 na kushika nafasi ya kwanza katika mkoa wa Iringa.

Kwa upande wake mwakilishi wa Mkuu wa Wilaya Mufindi Kaimu Katibu Tawala (DAS) Bwana Joseph Mchina ameipongeza Halmashauri ya mji wa Mafinga kwa kuwa na usimamizi mzuri wa utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo.

“Waheshimiwa Madiwani endeleeni kushirikiana na wataalamu hawa wa Halmashauri na wananchi kwa ujumla katika kufanikisha utekelezaji wa miradi yetu kwa viwango vyenye ubora unaotakiwa ambavyo thamani yake ya fedha inaonekana ili kuchochea maendeleo ya wananchi na kufikia kipato cha kati kwa manufaa ya sasa na ya kizazi kijacho” Alisema.

Matangazo

  • NAFASI ZA MASOMO KWA SHULE YA CHIEF MKWAWA ENGLISH MEDIUM- HALMASHAURI YA MJI MAFINGA. NAFASI BADO ZIPO TUPIGIE January 29, 2024
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA YANAPATIKANA www.mafingatc.go.tz July 13, 2024
  • MJI MAFINGA YAVUKA LENGO UKUSANYAJI MAPATO YAKUSANYA ASILIMIA 113 KWA MWAKA WA FEDHA 2023/2024 August 14, 2024
  • MATOKEO YA DARASAM LA SABA 2024 YANAPATIKANA KWENYE TOVUTI YETU .www.mafingatc.go.tz October 30, 2024
  • View All

Habari mpya

  • TUME HURU YA TAIFA YA UCHAGUZI IMEENDESHA MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA KWA AWAMU YA PILI JIMBO LA MAFINGA MJINI

    May 02, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 KATIKA HALMASHAURI YA MJI MAFINGA UMEPITIA JUMLA YA MIRADI 11 YA MAENDELEO YENYE THAMANI YA SHILINGI BILIONI 3.1

    May 01, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 KATIKA HALMASHAURI YA MJI MAFINGA UMEPITIA JUMLA YA MIRADI 11 YA MAENDELEO YENYE THAMANI YA SHILINGI BILIONI 3.1

    May 01, 2025
  • MBUNGE WA MAFINGA MJI AKABIDHI MITUNGI YA GESI

    May 01, 2025
  • View All

Video

SENSA NI MAENDELEO
Video zaidi

Viungo Vya Haraka

  • Maelezo na Form Ya kiapo cha uadilifu
  • https://matokeo.necta.go.tz
  • Muongozo wa matumizi ya TEHAMA serikalini

Tovuti Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya wananchi

Watembeleaji kidunia

world map hits counter

Idadi ya watu wanao tembelea Tovuti

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana na sisi

    Mafinga Town.

    Postal Address: Po.Box 76 Mafinga

    Simu: +255 262 772 393

    Mobile: 026-2772393

    Barua Pepe: td@mafingatc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Disclamer
    • Maswali
    • Sitemap
    • Huduma

Copyright ©2018 Mafinga Town Council . All rights reserved.